Irene Uwoya Awaonya Wanaopiga Picha za Nusu Uchi
Msanii wa filamu nchini Irene Uwoya na mke halali wa mwanamuziki Dogo Janja amefunguka na kuwataka ma-star wenzake kuacha kutumia 'skendo' za kupiga picha nusu utupu kwa madai vitendo hivyo vinamchukiza hadi Mungu na si TCRA pekee.
Uwoya ametoa kauli hiyo alipokuwa anazungumza kna eNewz ya EATV, na kusema wanaofanya na vitendo hivyo wanajidhalilisha wao wenyewe bila ya kujijua.
"Mimi nadhani kuna kitu watu hawajui au hawakitambui, kuwa kuna tofauti ya kutaka kuwa 'star' na kufanya kitu ambacho unakipenda ambacho kitakupelekea kuwa 'star' moja kwa moja", amesema Uwoya.
Pamoja na hayo, Uwoya ameendelea kwa kusema "mimi nawashauri watanzania kama kuna mtu anataka kuwa muigizaji basi afuate misingi iliyowekwa nasio kupiga picha za nusu utupu kwa kuwa haitoweza kumfanya mtu kuwa star na badala yake inakushusha. Wanaopiga picha za nusu utupu wanajidhalilisha kiukweli maana hata Mungu hapendi".
Kauli hiyo ya Irene Uwoya imekuja baada ya kupita takribani siku 36 tokea alipopigwa onyo na Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA), kuhusiana na kuchapisha picha za nusu utupu kwenye mitandao ya kijamii na kusisitiziwa kuwa endapo atarudia kufanya hivyo adhabu kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Mwanamke Atiwa Mbaroni Kwa Kumuua Mwanae na Mwingi kwa Kumuwekea Mwiko Sehemu za Siri
Wanawake
wawili wanashikiliwa na polisi mkoani Morogoro kwa tuhuma mbalimbali
akiwamo mmoja aliyemuua mtoto wake wa kiume wa miaka 11 kwa kumpiga
fimbo kichwani.
Katika
tukio jingine mwanamke mwingine anashikiliwa na polisi akituhumiwa
kumsokomeza mwiko sehemu za siri mtoto wa dada yake mwenye umri wa miaka
sita.
TCU: Kesho Ndo Mwisho wa Kutuma Maombi ya Kujiunga Chuo Kikuu Shahada ya Kwanza
Tume
ya vyuo Vikuu Tanzania (TCU) imesema kuwa kesho Agosti 15, 2018 ndiyo
mwisho wa kutuma maombi ya kujiunga na masomo ya shahada ya kwanza
katika vyuo vikuu na taasisi za elimu ya juu nchini.
Dirisha hilo la kuwasilisha maombi lilifunguliwa Julai 20, 2018 kwa awamu ya kwanza.
Akizungumza
leo Agosti 14, 2018 Katibu Mtendaji wa TCU Profesa Charles Kihampa
amesema kuwa baada ya kufungwa rasmi kwa dirisha la udahili vyuo
vitaanza kuchakata majina ya waombaji kulingana na vigezo vya udahili
vilivyowekwa kwa kila programu ya masomo.
Udahili
wa kujiunga na vyuo vikuu unahusu makundi makubwa matatu ambayo ni
waombaji wa kidato cha sita, wenye sifa linganifu kama vile shahada na
waombaji wenye vyeti toka nje ya nchi vyenye sifa linganifu.
"Baada ya kuchakata majina, dirisha la waombaji litaidhinishwa, " amesema Kihampa na kuongeza:
"TCU
jukumu lao ni kuhakiki kama waombaji waliochaguliwa na vyuo wana sifa
stahiki na wanakidhi vigezo vya kujiunga na programu husika za
masomo,"amesema Profesa Kihampa.
Amefafanua
kuwa waombaji wote wa udahili wanapaswa kutuma maombi yao moja kwa moja
kwenye vyuo wanavyopenda na kuchagua programu za masomo.
Amesema
Tume imetoa mwongozo wa programu zilizoidhinishwa kudahili pamoja na
vigezo vya udahili vinavyotakiwa kwa kila programu za masomo.
"Waombaji
wote wa vyuo vikuu na taasisi ya elimu ya juu wanakumbushwa na
kuhimizwa kuzingatia kalenda ya udahili iliyoidhinishwa na Tume,"amesema
Kihampa na kuongeza:
"Ili kuepusha usumbufu usio wa lazima, waombaji wote wanahimizwa kutumia muda uliobaki kukamilisha maombi yao.”
Wolper: Siwezi kudanga na siku nikikamata mmoja ni mimba tu
Msanii
wa Filamu Bongo, Jackline Wolper amesema kitu ambacho hawezi kufanya ni
kudanga. Wolper amefunguka hayo wakati akimjibu shabiki yake katika
mtandao wa Instagram kufuatia mrembo huyo kuposti picha ya Rais wa Kenya
na kuandika; My second home.
Sasa shabiki huyo alitupia comment yake kwenye post hiyo ambayo ilisomeka; "Siku Wakenya Watakukata ki******m ndo utajua ni second home au ni neighbor country we endeleaa tu kudangaaaa kwa waikikuyu"
Naye Jackline Wolper akajibu; "Siwezi
kudanga na siku nikikamata mmoja ni mimba tu usijali, halafu kasome
ujue maana ya kudanga.. na me kudanga siwezi, wanadanga watoto, am
sorry".
Jackiline
Wolper amekuwa nafari za mara kwa mara nchini Kenya kutokana na
biashara zake hasa ile ya ushonaji kupitia duka lake la House of
Stylish.















