Aliyenajisi binti wa miaka 9 Ahukumiwa Miaka 30 Jela

Aliyenajisi binti wa miaka 9 Ahukumiwa Miaka 30 Jela

Mahakama  ya Wilaya ya Ilala, imemhukumu Shabani Huseni (29), kifungo cha miaka 30 jela, baada ya kupatikana na hatia ya kunajisi mtoto wa miaka tisa.

Akisoma hukumu hiyo jana Hakimu Mkazi Catherine Kihoja alisema upande wa mashitaka ulipeleka mashahidi watano ambao wameweza kuthibitisha mashitaka bila kuacha shaka yoyote.

“Kutokana na ushahidi uliotolewa mahakamani hapa umeweza kuthibitisha mashitaka hivyo, mshitakiwa ninamtia hatiani kama alivyoshitakiwa,’’alisema Hakimu Kioja.

Kabla ya kutolewa kwa adhabu hiyo Wakili wa Serikali, Neema Moshi, aliomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mujibu wa sheria kwa kuwa mtoto aliyefanyiwa kitendo hicho ameathirika kisaikolojia na kupata madhara kiafya kutokana na kutokwa na harufu mbaya sehemu zake za siri.

Aidha, mshitakiwa aliomba mahakama impunguzie adhabu kwa kile alichodai kwamba hana ndugu, ombi ambalo lilitupiliwa mbali.

Inadaiwa kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo tarehe isiyofahamika Julai mwaka jana eneo la Kipunguni B, Moshi Baa wilayani Ilala ambapo alimbaka mtoto wa miaka tisa.
Share:

Related Posts:

1 comment:

Categories

Ordered List

  1. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  2. Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  3. Vestibulum auctor dapibus neque.

Sample Text

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua. Ut enim ad minim veniam, quis nostrud exercitation test link ullamco laboris nisi ut aliquip ex ea commodo consequat.

Definition List

Definition list
Consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.
Lorem ipsum dolor sit amet
Consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Pages