Tarime: Mkurugenzi Awatumbua Watumishi Wawili....Aapa Kumuwajibisha Yeyote Ataripotiwa wa Utovu wa Maadili

Tarime: Mkurugenzi Awatumbua Watumishi Wawili....Aapa Kumuwajibisha Yeyote Ataripotiwa wa Utovu wa Maadili

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Tarime, Elias Ntiruhungwa amewasimamisha kazi watumishi wawili wa halmashauri hiyo mbele ya kikao kwa madai ya kushindwa kufuata maadili ya kazi.

Waliosimamisha kazi ni, Jeveryson Kaguna kwa madai ya kushindwa kuandaa taarifa za watumishi kwa wakati zilizokuwa zinahitajika Ofisi ya Rais, zikiwamo za kupandisha madaraja na ongezeko la mishahara.

Mwingine aliyesimamishwa ni muuguzi wa Hospitali ya Wilaya ya Tarime, Kegosa Nega kwa madai ya kuwatukana wagonjwa hospitalini, utoro kazini na ukaidi. 

Mkurugenzi huyo aliwasimamisha kazi katika kikao cha watumishi wa halmashauri alichokiitisha kwa ajili ya kuwakumbusha wajibu wao na kufuata maadili ya kazi.

“Kuanzia sasa ninamsimamisha kazi ofisa utumishi kwa uzembe wa kushindwa kuandaa taarifa iliyokuwa inahitajika Ofisi ya Rais mwezi uliopita. Tuliambiwa tuandae majina ya watumishi wanaotakiwa kupanda madaraja waongezewe mishahara na kueleza mahitaji ya watumishi.

“Lakini hajaandaa na nilikuwa namkazania kila mara sasa sijui kama watu watapandishwa madaraja maana muda umeisha taarifa hazijakwenda,” alisema.

Kuhusu kusimamishwa kazi kwa muuguzi, alisema alikaidi agizo la mkubwa wake wa kazi la kumsaidia mgonjwa aliyekuwa amebebwa kwenye kitanda kumsukuma kumpeleka wodini.

Alisema hospitali ya wilaya imekuwa ikilalamikiwa kuwa baadhi ya watumishi hutoa kauli chafu kwa wagonjwa na kupokea rushwa kutoka kwa wagonjwa. 

Alisema mtumishi yeyote atakayeripotiwa kwa vitendo vya uvunjifu wa maadili atamuwajibisha.

 “Mtu anakwenda kazini kwa muda anaotaka yeye halafu ni wa kwanza kutoka kazini,” alisema Ntiruhungwa. 

Mratibu Elimu Kata ya Nyamisangura, Emanuel Mwihechi alisema suala hilo la watumishi kupandishwa madaraja ni muhimu, lakini kwa halmashauri ya mji limekuwa ni kero kwa watumishi kucheleweshewa madaraja.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Tarime, John Marwa aliwataka watumishi wote wa Serikali kutekeleza wajibu wao kwa kuzingatia sheria na taratibu za kazi ili kuepuka matatizo yanayoweza kuzuilika.

Share:

Related Posts:

No comments:

Post a Comment

Categories

Ordered List

  1. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  2. Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  3. Vestibulum auctor dapibus neque.

Sample Text

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua. Ut enim ad minim veniam, quis nostrud exercitation test link ullamco laboris nisi ut aliquip ex ea commodo consequat.

Definition List

Definition list
Consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.
Lorem ipsum dolor sit amet
Consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Pages