Mamlaka ya Bandari Bandari yapokea boti mbili za kuegesha meli

Mamlaka ya Bandari Bandari yapokea boti mbili za kuegesha meli

Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) imepokea boti mbili za kisasa za kuhudumia meli kutoka China zitakazotumika katika Bandari za Dar es Salaam na Tanga.

 Meneja Mawasiliano wa TPA, Janeth Ruzangi alisema ujio wa boti hizo zilizopolewa jana utasaidia kuongeza kasi ya utendaji kazi na ufanisi katika bandari hizo. 

Alisema ujio wa boti hizo ni sehemu ya mkakati wa TPA kuongeza vitendea kazi kwa upande wa majini na nchi kavu ili kuongeza kasi ya upakuaji na upakiaji wa mizigo kwa kiwango cha kimataifa na hivyo kuvutia wateja wengi. 

Nahodha Mkuu wa TPA, Kapteni Abdullah Mwingamno alisema boti ya tani 70 iliyopewa jina la Valeria Rugaihuruza itabaki Dar es Salaam kwa ajili ya kuhudumia meli zinazoshusha mafuta katika Boya la SPM lililopo Mji Mwema, wakati nyingine inayoitwa Mwambani itapelekwa Bandari ya Tanga kwa ajili ya kuhudumia matishari. 

Boti ya MV Valeria Rugaihuruza imeundwa na ‘crane’ yake pamoja na boti nyingine ndogo mbili ndani yake kwa ajili ya kusaidia utendaji kazi kwenye boya la mafuta. Boti ya MV Mwambani ina uwezo wa kuvuta tishari lenye uwezo wa kubeba tani 3,500 za mizigo.

Share:

Related Posts:

No comments:

Post a Comment

Categories

Ordered List

  1. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  2. Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  3. Vestibulum auctor dapibus neque.

Sample Text

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua. Ut enim ad minim veniam, quis nostrud exercitation test link ullamco laboris nisi ut aliquip ex ea commodo consequat.

Definition List

Definition list
Consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.
Lorem ipsum dolor sit amet
Consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Pages