Kidato cha Pili Waanza Mitihani leo

Kidato cha Pili Waanza Mitihani leo

Wanafunzi wa kidato cha pili nchini wameanza kufanya mitihani yao ya upimaji leo katika shule za sekondari 4,669 zilizopo Tanzania Bara.

Jumla ya wanafunzi 435,221 wamesajiliwa kufanya mitihani hiyo wakiwamo 67 wasioona na 306 wenye uoni hafifu.

Mbali na mitihani hiyo, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta), Dk Charles Msonde amesema mtihani wa Taifa wa darasa la nne utafanyika Novemba 23 na 24, mwaka huu.

"Mitihani hii inafanyika katikati ya mafunzo ili kubaini changamoto zilizopo na kutafuta namna ya kuboresha mafunzo hayo," amesema Dk Msonde.                      

Wakati huo huo, Dk Msonde amefafanua kuwa mafunzo ya ualimu wa shule ya msingi ngazi ya stashahada yamefutwa lakini wanafunzi waliopo vyuoni watamalizia masomo yao kwa muda uliobaki.

Dk Msonde amesema mafunzo hayo ya walimu yataendelea kwa utaratibu wa zamani ambao ulikuwa ngazi ya cheti.

Amesema usimamizi wa mitihani hiyo itakuwa chini ya Necta kama ilivyokuwa zamani badala ya Nacte.

"Wanafunzi walio vyuoni wataendelea na mafunzo hayo, isipokuwa kuanzia mwaka huu hatutadahili kwa ngazi ya diploma, tutadahili ngazi ya cheti kama ilivyokuwa zamani," amesema Dk Msonde. 
Share:

Related Posts:

No comments:

Post a Comment

Categories

Ordered List

  1. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  2. Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  3. Vestibulum auctor dapibus neque.

Sample Text

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua. Ut enim ad minim veniam, quis nostrud exercitation test link ullamco laboris nisi ut aliquip ex ea commodo consequat.

Definition List

Definition list
Consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.
Lorem ipsum dolor sit amet
Consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Pages