Clinton na Trump wapigania majimbo muhimu

Clinton na Trump wapigania majimbo muhimu


Hillary Clinton and Donald TrumpImage copyrightAFP
Hillary Clinton na Donald Trump wamezidisha kampeni zao, hasa kwenye majimbo yanayoshindaniwa sana, huku kura za maoni zikionesha wamekaribiana sana zikiwa zimesalia siku chache kabla ya uchaguzi mkuu.
Wawili hao kwa mara nyingine wameshambuliana kwenye mikutano ya kampeni, kila mmoja akisema mwenzake hafai kuwa rais.
Bi Clinton, ambaye uongozi wake kwenye kura za maoni kitaifa unaonekana kufutika siku za karibuni, amesema mpinzani wake wa chama cha Republican hawezi kudhibiti hisia zake na ana mtazamo hasi dhidi ya wanawake.
Bw Trump naye amesema Bi Clinton ataandamwa na uchunguzi wa jinai hadi ikulu ya White House.
Mgombea huo anaonekana kuimarika dhidi ya Bi Clinton katika majimbo yanayoshindaniwa, kwa mujibu wa kura za maoni.
Utathmini wa kura za maoni kitaifa kufikia tarehe 4 Novemba, 2016
Image captionUtathmini wa kura za maoni kitaifa kufikia tarehe 4 Novemba, 2016
Alhamisi, mkewe Melania alijitokeza kwenye mkutano wa kampeni kumtetea.
Kwenye hotuba yake ya kwanza tangu Julai wakati wa mkutano wa kitaifa wa chama cha Republican, mwanamitindo huyo wa zamani alizungumzia maisha yake kama mhamiaji na akasema mumewe ataifanya Marekani kuwa nchi ya haki.
Aidha, ameapa kuongoza kampeni dhidi ya watu kudhalilishwa na kudhulumiwa kwenye mitandao iwapo atakuwa mama wa taifa.
Akiongea kwenye viunga vya mji wa Philadelphia amesema atakabiliana na utamaduni ambao "umekuwa kaidi sana na katili".
Hata hivyo, hakuzungumzia tabia ya mumewe ya kuwashambulia na kuwatusi wapinzani wake kwenye mitandao ya kijamii.
Bw Trump ameimarika dhidi ya Bi Clinton katika majimbo kadha ya kushindaniwa, yakiwemo majimbo ya Florida na North Carolina, kwa mujibu wa kura za maoni.
Baadhi ya kura za maoni za kitaifa zinaonesha wawili hao wana kiwango sawa cha uungwaji mkono.
Makadirio ya utafiti wa Reuters/Ipsos yanaonyesha uwezekano wa Bi Clinton kushinda kura za wajumbe 270 zinazohitajika kushinda Jumanne kwa sasa ni 90% chini kutoka 95%.
Bw Trump ndiye anayeonekana kuimarika zaidi, na alifanyia hilo mzaha wikendi ya mwisho inapowadia.
Ametumia habari za FBI kuanzisha uchunguzi mpya kuhusu barua pepe za Bi Clinto kumshambulia zaidi mpinzani wake.
Melania TrumpImage copyrightAP
Image captionMelania Trump ameahidi kukabiliana na wanaoshambuliwa watu mitandaoni iwapo mumewe atashinda
"Ndio hao Wanaclinton tena - mwakumbuka vikao vya kumuondoa rais madarakani na matatizo mengine," Bw Trump aliambia waliohudhuria mkutano Jacksonville, Florida.
"Haya siyo mtayotaka, jameni. Twahitaji mtu aliye tayari kfuanya kazi."
Baadaye mkutano wa usiku Carolina Kaskazini, akizungumzia masuala ya ulinzi, alisema hawezi kutafakari Bi Clinton akiwa amiri jeshi mkuu.
Bi Clinton ameendelea kuangazia sifa za Bw Trump, na alisema Carolina Kaskazini: "Ametumia muda wake wote wa kampeni akiwapa filimbi wafuasi wake wenye chuki.
"Hili halijawahi kufanyika kwa mgombea wa chama kikubwa."
Pharrell Williams na Bernie Sanders wakiwa na Hillary ClintonImage copyrightREUTERS
Image captionPharrell Williams na Bernie Sanders wakiwa na Hillary Clinton
Aliongeza: "Iwapo Donald Trump atashinda uchaguzi tutakuwa na amiri jeshi mkuu ambaye hajielewi na ambaye mawazo yake ni hatari."
Rais Barack Obama amekuwa akitia bidii kumfanyia kampeni Bi Clinton, akijaribu kuwashawishi wapiga kura vijana na Wamarekani weusi wampigie kura.
Utathmini wa kura za mapema unaonesha huenda wapiga kura weusi hawajitokezi kwa wingi kupiga kura kama walivyofanya kumpigia kura Obama mwaka 2012.
Bi Clinton alipata nguvu zaidi pale mpinzani wake mkuu wa wakati wa mchujo Bernie Sanders alipojitokeza mkutano wake wa kampeni.
Kwenye mkutano huo Carolina Kaskazini Alhamisi jioni Bw Sanders alimsifu Bi Clinton kwa kujitolea kuinua ujira wa chini na kuangazia ukosefu wa usawa.
Nyota wa muziki Pharrell Williams pia alihudhuria na kumsifu Bi Clinton kwa kutetea haki za wanawake.
Share:

Related Posts:

No comments:

Post a Comment

Categories

Ordered List

  1. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  2. Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  3. Vestibulum auctor dapibus neque.

Sample Text

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua. Ut enim ad minim veniam, quis nostrud exercitation test link ullamco laboris nisi ut aliquip ex ea commodo consequat.

Definition List

Definition list
Consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.
Lorem ipsum dolor sit amet
Consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Pages