Hillary Clinton: Nilitaka kujificha kabisa

Hillary Clinton: Nilitaka kujificha kabisa


Hillary Clinton alitunukiwa heshima na wakfu wa Children's Defense Fund katika Newseum mjini Washington DC
Image captionHillary Clinton alitunukiwa heshima na wakfu wa Children's Defense Fund katika Newseum mjini Washington DC
Mgombea urais wa chama cha Democratic Hillary Clinton ameelezea masikitiko yake alipojitokeza hadharani mara ya kwanza tangu ashindwe kwenye uchaguzi wa rais nchini Marekani na Donald Trump wa chama cha Republican.
Bi Clinton, akihutubu mjini Washington DC amesema alikuwa hataki kutoka nyumbani tena.
Ameambia shirika la kuwasaidia watoto wasiojiweza kwamba uchaguzi huo umewafanya Wamarekani wengi kutafakari.
Bi Clinton aliongoza kwa wingi wa kura za kawaida lakini akashindwa kinyang'anyiro cha urais kupitia kura za wajumbe, ambazo ndizo huamua mshidni wa urais.
"Sasa, nitakiri kwamba kuja kwangu hapa halikuwa jambo rahisi," alisema alipokuwa akitunukiwa heshima na wakfu wa Children's Defense Fund.
"Kuna nyakati kadha wiki hiyo moja iliyopita ambapo nilitaka kujikunyata tu nikiwa na kitabu kizuri na nisiwahi kutoka nje ya nyumba tena."
Hillary ClintonImage copyrightGETTY IMAGES
Aliendelea: "Ninajua wengi wengu mmevunjwa moyo sana na matokeo ya uchaguzi. Hata mimi, pia, zaidi kushinda ninavyweza kueleza.
"Ninajua si jambo rahisi. Najua wiki moja iliyopita, watu wengi wamekuwa wakijiuliza iwapo Marekani ni nchi ambayo tumekuwa tukiamini ndiyo.
"Migawanyiko iliyowekwa wazi na uchaguzi huu imekolea, lakini tafadhali nisikezi ninaposema hili.
"Marekani ni ya thamani. Watoto wetu ni wa thamani. Kuweni na imani katika nchi yetu, mpiganie maadili yetu na daima, msikate tamaa."
Grey line
Alipokuwa anatoa hotuba ya kukubali kushindwa wiki iliyopita, Bi Clinton alsiema Bw Trump anafaa kupewa fursa ya kuongoza.
Tangu wakati huo, amekuwa haonekani, ingawa siku moja alionekana akifanya matembezi porini.
Mfuasi wa ClintonImage copyrightFRANK FRANKLIN II / AP
Image captionBi Clinton alishinda ngome za Democratic California, Oregon, New York, New Jersey, Connecticut, Massachusetts, Maryland, Vermont, Delaware, Illinois, Rhode Island, Hawaii, Washington na District of Columbia, pamoja na New Mexico na Colorado.
Kwenye mawasiliano ya simu ambayo yalifichuliwa kwa wanahabari Marekani, alisikika akimlaumu mkurugenzi mkuu wa FBI James Comey, aliyetangaza kuanzishwa kwa uchunguzi mpya kuhusu kashfa yake ya barua pepe zikiwa zimesalia siku 11 kabla ya uchaguzi mkuu kufanyika.
Baadaye uchaguzi ulipokuwa umekaribia kabisa, Bw Comey alisema hakukupatikana ushahidi mpya ambao ungebadilisha uamuzi wa awali wa FBI kwamba hakukuwa na ushahidi wa kumfungulia mashtaka.
Share:

Related Posts:

No comments:

Post a Comment

Categories

Ordered List

  1. Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  2. Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  3. Vestibulum auctor dapibus neque.

Sample Text

Lorem ipsum dolor sit amet, consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua. Ut enim ad minim veniam, quis nostrud exercitation test link ullamco laboris nisi ut aliquip ex ea commodo consequat.

Definition List

Definition list
Consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.
Lorem ipsum dolor sit amet
Consectetur adipisicing elit, sed do eiusmod tempor incididunt ut labore et dolore magna aliqua.

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Pages